Isimu Linganishi na Tofautishi: Mfanano na Tofauti

Main Article Content

Ibrahim Elhadi M. Lehmedi 1
Mohammed younis Khalifa 2

Abstract

Utafiti huu unachunguza kwa kina taaluma za isimu linganishi na isimu tofautishi, ukibainisha mfanano na tofauti zao muhimu katika uwanja wa isimu ya kisasa. Isimu linganishi, ambayo ni mbinu kongwe zaidi, inalenga kurejesha lugha mama za kale kupitia kulinganisha lugha zenye asili moja, huku ikifichua uhusiano wa kihistoria na mageuzi ya lugha. 
Isimu tofautishi, tawi la isimu tumizi, inalinganisha lugha mbili au zaidi za kisasa, bila kujali asili yao, kwa lengo la kubainisha tofauti na mfanano wa kimfumo ili kurahisisha matatizo ya kufundishak na kuujifunza lugha ya pili. Utafiti huu unachambua historia ya taaluma hizi, misingi yake ya kinadharia,mbinu zinazotumika, na umuhimu wake katika kuelewa lugha na kuboresha mbinu za kufundishia. Pia, unajadili mchango wa wataalamu wa lugha katika kuanzisha misingi ya isimu linganishi na tofautishi huku ukisisitiza umuhimu wa kuendeleza tafiti za kisasa katika lugha ya Kiarabu na Kiswahili.

Downloads

Download data is not yet available.

Article Details

Section

Articles